Jinsi unavyoweza kutumia MyPlanKenya kwa usalama:

Unapotumia MyPlanKenya au raslimali zingine, hakikisha kuwa unaweza kufanya hivyo kwa usalama na kwa usiri. Hapa kuna maagizo ya jinsi ya  kutumia mtandao kwa usalama.

Kwa kutumia "Usiri" au Hali Fiche:

Unapotumia MyPlanKenya kwenye mtandao, utahitaji kutumia kifaa cha siri. Hii pia inaitwa kwenda "kwa hali fiche". Ikiwa umefungua kurasa fiche, hiyo inamaanisha kuwa kila kitu unachofanya na kutafuta ndani ya kurasa hiyo kitafutwa mara tu utakapofunga ukurasa huo.

MyplanKenya inapendekeza kutumia hali fiche kila wakati unapo tumia raslimali zetu.

Tazama hapa chini kwa maagizo ya jinsi ya kutumia hali fiche/ya siri kwenye chombo chako cha kuingia kwenye mtandao.

 

Google Chrome

Kwenye Kompyuta yako

1)      Kwenye kompyuta yako, fungua Chrome

2)      Sehemu ya juu ya kulia, bonyeza “Zaidi”  Ukurasa mpya Fiche

3)      Ukurasa mpya utaonekana. Katika kona ya juu kulia, angalia aikoni ya hali fiche:

 

Unaweza pia kutumia njia ya mkato ya kibodi kufungua ukurasa fiche:

                Kwenye Windows, Linus, au Chrome Os: Bonyeza Ctrl + Shift + n

                Kwenye Mac: Bonyeza  + Shift + n

 

Kwenye iPhone ama iPad

1)      Kwenye  iPhone yako  ama iPad, fungua programu ya Chrome

2)      Bonyeza “Zaidi”  Ukurasa mpya Fiche

Kuhakikisha kuwa uko katika Hali Fiche, gusa "Badilisha  kibonyezo" . Telezesha kidole kulia ili uone ikiwa una kurasa za maelezo ya hali fiche ilivyo wazi. Katika sehemu ya juu, tafuta ikoni ya hali fiche

Kwenye Android

1)      Kwenye simu yako au kwenye skrini ya simu fungua alama ya chrome

2)      Kwenye upande wa kulia bonyeza "zaidi"  Ukurasa fiche

3)      Ukurasa mpya unafunguka kwenye upande wa juu wa kushoto, angalia aikoni ya ukurasa fiche

 

 

Safari

1)      Fungua  Safari kwenye kompyuta, simu, au ipad

2)      Bonyeza kwenye ''ukurasa''

3)      Bonyeza [nambari] kwenye ukurasa  kuonyesha ukurasa wa orodha ya vikundi

4)      Bonyeza"siri", kisha bonyeza" Kamilika"

 

Ukiwa katika mtandao wa hali fiche, mstari wa Safari unakuwa na rangi nyeusi au ya giza badala ya kuwa nyeupe au kijivu.

 

Opera

1)      Fungua Opera  

2)      Bonyeza doti tatu

3)      Bonyeza hali fiche

 

Kufuta historia yako ya matumizi kwa mtandao:

Njia nyingine ya kuweka usiri katika shughuli yako ya matumizi katika mtandao, ni kufuta historia yako ya matumizi mtandaoni. Kwa kufanya hivyo, historia yote ya sehemu ulizopitia pamoja na 'cookies' na 'cache' ambazo ni njia zingine  za kuweka habari zitafutwa.

MyPlanKenya inapendekeza kufuta historia yako ya matumizi mtandaoni kila wakati baada ya kutumia rasilimali zetu.

Tazama hapa chini kwa maagizo ya jinsi ya kufuta historia ya matumizi yako mtandaoni.

 

Google Chrome

Kwenye kompyuta

1)      Kwenye kompyuta yako, fungua Chrome

2)      Juu upande wa kulia bonyezazaidi Mipangilio

3)      Bonyeza Historia > Historia.

4)      Upande wa kushoto, bonyeza futa za  habari za mtandaoni. Kijisanduku kitaonekana.

5)      Kutoka kwa mpangilio wa orodha, chagua idadi ya historia unayotaka kufuta. Kufuta kila kitu, chagua kila wakati.

6)      Chagua vijisanduku kwa maelezo unayotaka kufuta kutumia chrome pamoja nahistoria ya matumizi mtandaoni”, “cookies na habari ya tovuti”, napicha na faili zilizohifadhiwa”.

7)      Bonyeza futa habari.

Kwenya iPhone ama iPad

1)      Kwenye iphone ama ipad yako,fungua programu ya Chrome

2)      Bonyeza “Zaidi” Historia

3)      Hapo china, bonyeza futa habari ya matumizi mtandaoni.

4)      Chagua habari ya maelezo unayotaka kufuta, pamoja nahistoria ya matumizi mtandaoni”, “cookies na habari ya tovutinapicha na faili zilizohifadhiwa”.

5)      Bonyeza futa habari ya matumizi mtandaoni > futa habari ya matumizi mtandaoni.

6)      Kwa upande wa juu wa kulia, bonyeza Kamilika.

 

Kwenye Android

1)      Kwenye simu yako ya Android au tablet, fungua programu ya Chrome

2)      Bonyeza ''zaidi''  Mipangilio

3)      Bonyeza, usiri na usalama > futa habari za matumizi mtandaoni.

4)      Kufuta kila kitu, chagua kila wakati.

5)      Chagua habari ya maelezo unayotaka kufuta, pamoja nahistoria ya matumizi mtandaoni”, “cookies na habari ya tovutinapicha na faili zilizohifadhiwa”.

6)      Bonyeza futa habari.

 

Safari

1)      Fungua Safari

2)      Enda kwa mipangilio

3)      Tafuta programu ya “Safari”

4)      BonyezaFuta historia na habari ya mtandao

Ikiwa hakuna historia au habari ya tovuti ya kufuta, mpangilio hua kijivu. Mpangilio unaweza pia kuwa kijivu ikiwa una kizuizi cha kuona maelezo ya tovuti yalio undwa chini ya maelezo ya vizuizi vya usiri kwenye skrini: Content & Privacy Restrictions in Screen Time.

 

Opera

1)      Fungua Opera

2)      Bonyeza Ctrl+H kufungua ukurasa wa historia yako

3)      Bonyeza Futa maelezo ya matumizi mtandaoni kwenye kona ya juu ya kulia

4)      Chagua unachotaka kufuta na muda kama, “kila wakati

5)      Bonyeza Futa habari